RUSA yakashifu wizi wa mifugo Kambinye
Na Sabalua Moses
Muungano wa wanafunzi wa vyuo vikuu kutoka jamii ya Rendille chini ya chama cha (RUSA) umekashifu vikali tukio la wizi wa mifugo lililotokea wiki iliyopita katika eneo la Kambinye, wadi ya Kargi.
Wakizungumza na wanahabari, naibu mwenyekiti wa chama hicho Jordan Sahado amesema kuwa wizi wa mifugo ni uhalifu usio na kabila, akisisitiza kuwa hakuna mila yoyote inayounga mkono vitendo vya wizi wa mifugo.
Sahado pia amelaani uharibifu wa mali na mifugo uliosababishwa na tukio hilo, akieleza kuwa uhalifu huo umeathiri pakubwa maisha ya wafugaji wanaotegemea mifugo kama njia kuu ya kujikimu katika eneo hilo.



Post Comment