Papa Leo XIV amteua Padri John Mbua Mwandi kuwa Askofu msaidizi wa Jimbo Katoliki la Kitui
Waamini wa Kanisa Katoliki nchini Kenya wamepokea kwa furaha uteuzi wa Padri John Mbua Mwandi kuwa Askofu msaidizi wa Jimbo Katoliki la Kitui, baada ya tangazo rasmi kutoka Vatican kupitia Ofisi ya Vyombo vya Habari vya Holy See.
Hadi uteuzi wake Padri John Mbua alikuwa Padri mkuu wa Parokia ya Mulutu.
Askofu Mteule John Mbua Mwandi alizaliwa tarehe 24 Septemba 1970. Alisoma falsafa katika Seminari Kuu ya Saint Augustine iliyoko Jimbo katoliki la Bungoma, na baadaye akasomea theolojia katika Seminari Kuu ya Saint Matthias Mulumba iliyoko Kapsabet.
Alipadrishwa tarehe 8 Desemba 2001.
Baada ya kupadrishwa, Askofu Mteule Mwandi alihudumu katika nyadhifa mbalimbali ndani ya Kanisa. Alianza kama Paroko Msaidizi wa Ikutha mwaka 2002, kisha akawa Paroko wa Miambani, Ikanga, na baadaye Kanisa Kuu (Cathedral) ya Kitui.
Katika huduma yake ya kichungaji, alihitimu stashahada ya Usimamizi wa Miradi kutoka Kenya Institute of Management, Nairobi, mwaka 2008. Kuanzia mwaka 2011 hadi 2020, alihudumu kama Mhasibu wa Jimbo kisha akaendelea kuwa vika jenerali wa Jimbo Katoliki la Kitui.



Post Comment