Highlights

Mwanaume mmoja ahukumiwa kifungo cha maisha gereza kwa kumlawiti mvulana wa miaka 6, Marsabit Central

Mahakama ya Marsabit imemhukumu mwanaume mmoja kifungo cha maisha gerezani kwa kupatikana na hatia ya kumlawiti mvulana wa umri wa miaka 6, katika eneo la Township kaunti ndogo ya Marsabit Central.

Mhukumiwa Roba Tura amepatikana na hatia ya kumlawiti mtoto huyo mnamo tarehe 8 mwezi April 2025.

Akitoa hukumu hiyo leo Jumatano Hakimu Mkuu Mwandamizi wa mahakama ya Marsabit Christine Wekesa amesema kuwa ushahidi uliyowasilishwa mahakamani umebaini kuwa Roba alimlawiti mvulana huyo ambaye kipindi hicho alikuwa mtoto wa kurandaranda mitaani.

Mwanaume huyo anasiku 14 kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo.

Radio Jangwani 106.3FM is a community radio station situated in Marsabit County broadcasting from Marsabit town. It is the brain child of the bishop of catholic diocese of Marsabit, Rt. Rev. Peter Kihara. It is established with the objective of reaching the people Marsabit diocese and Marsabit County for evangelization, Education, entertaining and disseminating information to the masses.

Post Comment