Mwalimu afikishwa mahakamani kwa tuhuma za kumnajisi mwanafunzi Kargi.
Na Mwandishi wetu
Mwalimu aliyekamatwa wiki jana kwa tuhuma za kumnajisi mwanafunzi wa miaka 14 katika kaunti ndogo ya Loiyangalani, amefikishwa katika mahakama ya Marsabit Leo Jumatatu.
Mshukiwa Dennis Kipkoech Chepkwony amefikishwa mbele ya hakimu Edward Oboge ambapo pia ameshtakiwa kwa kosa la kumshika visivyo mwanafunzi huyo.
Mshukiwa anadaiwa kutekeleza kosa hilo kati ya tarehe 5 hadi 18 mwezi Aprili mwaka 2026.
Hakimu ameagiza idara ya probesheni kuwasilisha ripoti kutathmini iwapo mshukiwa anaweza kuachiliwa kwa bondi au la.
Kesi hiyo itatajwa tarehe 8 mwezi Juni.



Post Comment