Highlights

Mshukiwa wa ulawiti asakwa Logo Logo.

Na Nyabande Orwa

Maafisa wa usalama wanaendelea kumsaka mshukiwa wa tukio la kulawiti lililoripotiwa katika eneo la Logo Logo, kaunti ya Marsabit.

Kwa mujibu wa chifu wa Logo Logo, Andrew Korolle, mshukiwa anayekadiriwa kuwa na umri wa takriban miaka 16 alitoroka baada ya kumlawiti mvulana wa miaka 10 walipokuwa malishoni siku ya Jumapili.

Korolle amesema kuwa wakazi waliokuwa malishoni wakichunga mifugo ndio walioshuhudia tukio hilo na kutoa taarifa kwa ofisi ya chifu.

Kwa sasa, mtoto aliyeathiriwa anapatiwa matibabu katika hospitali ya Laisamis.

Wakati huo huo, chifu huyo amewataka wazazi kufuatilia mienendo ya watoto wao ili kusaidia kuzuia matukio kama hayo. Pia amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha watoto waliofikia umri wa kwenda shule wanahudhuria masomo badala ya kupelekwa malishoni.

Aidha, amewahimiza wananchi kutoa taarifa kwa vyombo vya usalama wanaposhuhudia visa kama hivi ili hatua za kisheria ziweze kuchukuliwa.

Radio Jangwani 106.3FM is a community radio station situated in Marsabit County broadcasting from Marsabit town. It is the brain child of the bishop of catholic diocese of Marsabit, Rt. Rev. Peter Kihara. It is established with the objective of reaching the people Marsabit diocese and Marsabit County for evangelization, Education, entertaining and disseminating information to the masses.

Post Comment