Highlights

Gavana Mohamud Ali ahidi kutoa mazingira bora kwa  biashara za vijana Marsabit.

NA JB Nateleng

Gavana wa kaunti ya Marsabit, Mohamud Ali, amewahakikishia vijana waliopata mtaji wa kuanzisha biashara kupitia mradi wa NYOTA kuwa serikali ya kaunti itabuni mazingira bora ya kuendesha biashara zao kwa usahihi na usawa.

Akizungumza katika hafla ya utoaji wa fedha iliyoongozwa na Rais William Ruto katika Kituo cha Archers Post, Kaunti ya Samburu, Gavana Mohamud amesema kaunti ipo imara kuhakikisha vijana hao wanapata mafunzo ya kutosha na muda wa kutosha wa kuendesha biashara zao kwa njia salama na yenye tija.

Aidha, amefutilia mbali ada ya leseni ya mwaka mmoja kwa vijana hawa na kuahidi ushirikiano zaidi wa kaunti ili kuwasaidia kiuchumi.

Radio Jangwani 106.3FM is a community radio station situated in Marsabit County broadcasting from Marsabit town. It is the brain child of the bishop of catholic diocese of Marsabit, Rt. Rev. Peter Kihara. It is established with the objective of reaching the people Marsabit diocese and Marsabit County for evangelization, Education, entertaining and disseminating information to the masses.

Post Comment