Wanaoendeleza ukeketaji Marsabit waonywa
NA JAMES MUCHAI
Watu wanaoendeleza ukeketaji katika kaunti ya Marsabit wameonywa vikali dhidi ya kuendelea kutekeleza tamaduni hiyo iliyopitwa na wakati.
Akizungumza na wanahabari habari mjini Marsabit, Naibu mwenyekiti wa amani katika kaunti hii, Adan Chukulisa, amesema kuwa yeyote atakayepatikana akijihusisha na kitendo hicho atachukuliwa hatua kali za kisheria.
Aidha, Chukulisa amewataka wazazi kuwachunga na kuwalinda watoto wao msimu huu wa likizo ndefu, huku akionya kuhusu hatari ya dawa za kulevya. Ameeleza kuwa walimu wametekeleza jukumu lao wakati wa muhula wa masomo, na sasa ni wajibu wa wazazi kuhakikisha usalama na malezi bora ya watoto wao.
Amesisitiza pia umuhimu wa vijana kujiepusha na dawa za kulevya, uhalifu na uhasama, akiwashauri kujihusisha na masuala ya michezo ili kujijenga kimwili na kiakili.



Post Comment