Loading Now

Highlights

Polisi waimarisha oparesheni ya kuwarejesha mifugo walioibiwa eneo la Moite.

NA HENRY KHOYAN

Polisi wamethibitisha kuwa wameimarisha oparesheni ya kusaka mifugo iliyoporwa katika eneo la Moite wiki iliyopita.

Takriban wiki moja baada ya wizi huo, maafisa wa usalama kwa kushirikiano na jamii za eneo hilo wanaendelea na msako dhidi ya wahalifu na mifugo hiyo.

Naibu Kamishna wa kaunti ndogo ya North Horr, Tobias Onyango Okoth, amesema jamii husika imeomba hadi Jumapili ili kusaidia kufanikisha upatikanaji wa mifugo hiyo.

Aidha, Okoth amesema wezi hao huenda wamejigawa sehemu mbili, na polisi bado wanaendelea kuwafuatilia kwa karibu ili kuhakikisha mifugo inarejeshwa kwa usalama.

Radio Jangwani 106.3FM is a community radio station situated in Marsabit County broadcasting from Marsabit town. It is the brain child of the bishop of catholic diocese of Marsabit, Rt. Rev. Peter Kihara. It is established with the objective of reaching the people Marsabit diocese and Marsabit County for evangelization, Education, entertaining and disseminating information to the masses.

Post Comment