Sport Bulletins

Michuano Ya Kuwania Kombe La Ligi Kuu Nchini Uingereza Kuendelea Usiku Wa Leo.

Picha;Hisani.

By Waihenya Isaac.

Michuano Ya Kuwania Kombe La Ligi Kuu Nchini Uingereza Inatarajiwa Kuendelea Usiku Wa Leo Huku Mechi Tatu Zikiratibiwa Kugaragazwa.

Sheffield United Ya Kocha Chris Wilder Itasaka Ushindi Wake Wa Kwanza Msimu Huu  Baada Ya Kupoteza Mechi Kumi Na Tano Kati Ya Kumi Na Saba Walizocheza Msimu Huu, Itakapomenyana Na Newcastle United Ugani  Bramall Lane Kuanzia Saa Tatu Usiku.

Itimiapo Saa Tano Usiku Vijana Wa Ole Gunnar Manchester United Watatafuta Nafasi Ya Kupanda Kileleni Mwa Jadwali La EPL Kwa Mara Ya Kwanza Msimu Huu Watakapovaana Na Burnely Ugani Turf Moor.

United Wanashilikia Nafasi Ya Pili Kwa Alama 33, Alama Sawa Na Viongozi Liverpool Ambao Wamecheza Mechi Moja Zaidi.

Mida Io Hiyo Wolves Baada Ya Kulazimisha Sare Ya Goli Moja Kwa Moja Weekend Iliyopita Dhidi Ya Brighton And Hove Atakuwa Mwenyeji Wa Everton Ugani Molineux Stadium.

Subscribe to eNewsletter