Sport Bulletins

Mechi kati ya Manchester United dhidi ya Brentford yaahirishwa.

Picha:Hisani

Na Waihenya Isaac,

Mchuano wa kuwania kombe la ligi kuu nchini Uingereza kati ya Manchester United dhidi ya Brentford imeahirishwa kutokana na mkurupuko wa visa vya korona katika kambi ya Man United.

Kupitia Kurasa zao za kijamii vilabu vyote viwili vimedhibitisha kuahirishwa kwa mechi hiyo iliyotarajiwa kusakatwa hii leo usiku ugani Old Trafford hadi tarehe nyingine.

Ujumbe kutoka ukurasa wa Twitter wa Brentford Ulisema kuwa klabu hiyo inawatakia wote walioathirika afueni ya haraka na tunatarajia kukutana nao Mwaka Mpya.

Mapema hiyo jana Klabu ya Manchester United ilitoa ripoti rasmi kuhusia na kuwepo kwa visa vya korona kambini mwao japo idadi ya walioambukizwa virusi hivyo haikutajwa.

Subscribe to eNewsletter