Sport Bulletins

Chelsea Yawazia Kumsajili Nyota Wa Barcelona Lionel Messi

Photo: Courtesy

By Waihenya Isaac,

Klabu Ya Chelsea Imeripotiwa Kuwa Makini Kupata Huduma Za Mchezaji Nyota Wa Argentina Na Barcelona Lionel Messi Msimu Ujao Wa Majira Ya Joto Mwakani.

Inaarifiwa Kuwa Chelsea Wamekuwa Wakifuatilia Kwa Karibu Hali Ya Messi Na Miamba Hao Wa La Liga.

Haya Yanajiri Miezi Michache Tu Baada Ya Nyota Huyo Mwenye Umri Wa Miaka 33, Kufahamisha Uongozi Wa Barcelona Mnamo Mwezi Agosti Mwaka Huu, Kuwa Anataka Kuondoka Klabu Hiyo Ila Hatua Za Kuondoka Hazikufaulu.

Hali Ya Messi Ugani Camp Nou Imekuwa Ya Atiati Tangu Klabu Hiyo Kulazwa Na Bayern Munich Magoli 8 – 2 Katika Awamu Ya Robo Fainali Mechi Ya Klabu Bingwa Ulaya.

Subscribe to eNewsletter