County Updates, Diocese of Marsabit

Baadhi Ya Walimu Wakuu Katika Shule Za Misingi Za Marsabit Watoa Hisia Zao Kuhusiana Watahiniwa Wa KCPE Kutakiwa Kujiunga Na Shule Ya Kutwa Zilizoko Katika Kaunti Zao.

Picha :Hisani

By Mark Dida,

Baadhi ya walimu wakuu wa shule ya misingi eneo hili wametoa hisia mbali mbali baada Katibu katika Wizara ya Elimu Belio Kipsang kutoa tarifa kuwa watahiniwa wa KCPE wanatakiwa kujiunga na shule ya kutwa zilizoko katika kaunti zao.

Kuligana na mwalimu wa shule ya msingi St. John Memorial Charles Stephen, wazo hilo ni zuri kwani ni njia bora ya kukabiliana na kuenea kwa virusi vya corona.

Aidha ameogeza kuwa ni huenda ikasaidia wazazi kuchunguza nidhamu ya wanao wakati huu ambapo wanafunzi wanazua rabsha shuleni.

Aidha, wengine wametoa hisia tofauti huku wakisema kuwa ni changamoto kwa wanafunzi walio na maono ya kujiunga na shule bora zaidi nchini.

Walimu hawa wameambia Radio Jangwani kuwa muda wa kudurusu na kufanya mabadiliko ya kujaza fomu pia ni chanagamoto kubwa wakti ambapo wanatayarisha wanafunzi kwa mitihani ya KCPE ya mwaka huu.

Itakumbukwa kuwa wizara ya ilimu imeagiza walimu wakuu na wakurugenzi wa elimu wa mikoa na wale wa kaunti ndogo kuhakikisha wanafuzi wanadurusu fomu hiyo kuanzia tarehe 16 mwezi wa febuar hadi 26.

Subscribe to eNewsletter