Itakua vigumu kwa rais Ruto kupata muhula wa pili iwapo hatatimiza ahadi zake
May 12, 2025
NA Sebalua Moses
Ripoti ya wizara ya afya nchini imesema kuwa kuna ongezeko la matumizi ya mihadarati miongoni mwa vijana huku mmoja kati ya vijana 11 ni mraibu wa dawa za kulevya.
Ripoti hiyo pia imeorodhesha pombe, miraa pamoja na sigara kama dawa za kulevya ambazo hutumika zaidi mno.
Mwanahakarati wa kupinga matumizi ya dawa za kulevya katika kaunti ya Marsabit Fred Ochieng amesema kuwa matumizi ya dawa ya kulevya miongoni mwa vijana nchini iko juu zaidi.
Hata hivyo Ochieng ametoa wito kwa wazazi kushirikiana kwa pamoja ili kusaidia watoto wao sawa na kuwataka wazazi kuwa mfano mzuri ili watoto wasiige tabia zao
Wakati huo mwanaharakati huyo amesema ni sharti washirikiane kwa pamoja kwani ni jukumu la kila mtu katika kaunti ya Marsabit kusaidia katika kupambana na kero hilo la matumizi ya dawa za kulevya miongoni mwa vijana