County Updates, Local Bulletins

WALIMU WATAKIWA KUWA NA SUBIRA KUHUSIANA NA BIMA YA (SHA) HUKU TSC IKISAKA SULUHU YA BIMA HIYO KWA WALIMU.

Na JB Nateleng

Walimu wametakiwa kuwa na subira kuhusiana na suala la bima ya Afya huku tume ya kuajiri walimu TSC ikishirikisha washikadau kutoka Mamlaka ya Afya ya Jamii (SHA)  ili kutatua utata uliopo.

Kulingana na katibu wa chama cha kutetea maslahi ya walimu KUPPET tawi la Masabit Sarr Galgalo ni kwamba tume ya Kuajiri walimu TSC inashughulikia suala hilo huku akiwarai walimu kuweza kutembelea hospitali ili kupata huduma ya afya panapohitajika kwa sababu  makato ya hapo awali ya NHIF yamehamishwa kwa SHA

Sarr ameelezea kwamba mvutano huu umesababishwa na mamlaka ya afya ya Jamii SHA kuitisha fedha nyingi kuliko ya bima ya Minet ambayo ilikuwa ikifadhili matibabu ya walimu.

Sarr ameitaka TSC kuzungumza na mratibu wa Bajeti ili kuharakisha mchakato wa kuwahamisha bima ya afya ya walimu kutoka Minet mpaka SHA.

Subscribe to eNewsletter