County Updates, Local Bulletins

WAKENYA WACHACHE HUSHIRIKI KATIKA KUWEKEZA AKIBA YAO KWA SABABU YA MIKOPO YA DIGITALI

Picha Hisani

Imebainika kuwa wakenya wanakopa zaidi ya shilingi millioni 500 kwa siku na shilingi billioni 15 kwa mwezi  kwa mujibu wa ripoti iliyotolewa na shirika la Digital  Financial services Association of Kenya (DFSAK).

Mtaalam wa masuala ya kifedha katika kaunti ya Marsabit John Maina  katika  amesema kuwa ongezeko hilo la kuchukua mikopo ya digitali imechangiwa na  kuongezeka kwa gharama ya maisha  pamoja na kucheleweshwa kwa mishahara ya wafanyakazi haswa walioajiriwa kwenye mashirika ya kibinafsi na serikali za kaunti .

Kulingana na Maina Ripoti  hiyo  imeeleza kuwa zaidi ya wakenya millioni 8  wanatumia njia ya digitali kuchukua mikopo hiyo..

Aidha John amesema kuwa mikopo hiyo ya digitali imewafanya wakenya kutowekeza katika akiba zao hiyo kufanya maisha kuwa magumu zaidi.

Subscribe to eNewsletter