County Updates, Local Bulletins

VIJANA WATAKIWA KUJIUNGA NA SHULE ZA KIUFUNDI KATIKA KAUNTI YA MARSABIT ILI KUWEZA KUJIAJIRI.

Na Sebalua Moses

Vijana katika kaunti  ya Marsabit wametakiwa kujiunga na vyuo vya kiufundi ili kupata ujuzi wa kujiajiri. Haya ni kwa mujibu wa afisa mkuu katika idara ya elimu kaunti ya Marsabit Robert Mugambi.

Akizungumza na shajara ya radio jangwani Mugambi amesema kuwa vijana humu nchini wana nafasi kubwa ya kujiendeleza   katika jamii  na kwa hiyo ni sharti wajielimishe na hata kujitafUtia ajira ambazo zitaweza kukimu mahitaji yao kupitia mafunzo yanayotolewa katika   vyuo vya kiufundi. Mugambi Pia amesema kuwa Kaunti  ya Marsabit ina vyuo vya kiufundi vya kutosha.

Vile vile Mugambi amewataka vijana kuwa mstari wa mbele katika kujiunga na vyuo vya kiufundi haswa wakati huu shule zinapofunguliwa. Aidha amesema kuwa ni sharti vijana waweze kujitaftia ajira kupitia kwa mafunzo wanazopata katika vyuo vya kiufundi  huku akiwahimiza kutokaa manyumbani kungoja nafasi  za kazi kutokea .

Wakati huo huo Mugambi amesema  kaunti ya Marsabit imeweka mikakati ya kutosha na kuboresha elimu ya vyuo  vya ufundi akiwahimiza vijana kuwa watapokea mafunzo hayo bila malipo

 

Subscribe to eNewsletter