Itakua vigumu kwa rais Ruto kupata muhula wa pili iwapo hatatimiza ahadi zake
May 12, 2025
Na Caroline Waforo
Maafisa wa polisi katika eneo la Moite wadi ya Loiyangalani kufikia wamefanikiwa kurejesha ngamia wanane waliokuwa wameibiwa ya Alhamisi iliyopita na wezi wa mifugo.
Akithibitisha kisa hicho naibu kamanda wa polisi katika kaunti ndogo ya Loiyangalani Nicholas Mutua, ambaye amezungumza na Shajara ya Radio Jangwani kwa njia ya simu, amesema kuwa wahalifu waliiba mifugo hao waliokuwa wakichungwa na watoto.
Anasema kuwa kurejeshwa kwa ngamia hao 8 kati ya 16 waliokuwa wameibiwa imefanikishwa kwa ushirikiano na naibu kamanda wa kaunti ndogo ya North Horr
Mutua ameendelea kutoa tahadhari kwa wazazi dhidi ya kuwapa watoto wadogo majukumu ya kulisha mifugo haswa maeneo ya mbali hususan msimu huu wa likizo ndefu ya mwezi Aprili akisema kuwa pia inahataraisha maisha yao.
Mutua amesema kuwa wanaendelea kuwasaka ngamia waliosalia huku akiwahakikishia wakaazi wa eneo hilo usalama wa kutosha akisema kuwa wameimarisha doria katika kaunti ndogo ya Loiyangalani.