County Updates, Local Bulletins

AFUENI KWA WANAOTUMIA BARABARA YA SARIMA NAKUROL – LOIYANGALANI BAADA YA KENHA KUAHIDI KUIKARABATI.

Na Joseph Muchai

Mwakilishi wadi wa Loiyangalani Musa Daniel Ejomo amewata wakaazi wa eneo hilo kuwa na Subira wakati huu KENHA inapojiandaa kuikarabati barabara ya Sarima Nakurol kuelekea Loiyangalani.

 Akizungumza na vyombo vya habari, MCA Emojo amesema kuwa amewasiliana na mkurugenzi wa mamlaka ya barabara kuu nchini KENHA wa ukanda wa mashariki ya juu Norbat Momanyi na kukubaliana kuwa shughuli hiyo itang’oa nanga hivi karibuni.

Aidha Emojo vilevile amesema kuwa barabara hiyo imekuwa na tatizo kupitika haswa maeneo ya Nakurol kutokana na kufura kwa ziwa Turkana.

Hata hivyo amewarai waendesha magari kutafuta njia mbadala kwani kuna sehemu iliyochimbika kutokana na mafuriko hayo.

Subscribe to eNewsletter