Mwanaume moja wa miaka 38 ameponea kifo baada ya jaribio la kujitoa uhai kwa kujinyonga kutibuka usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Soweto mjini Laisamis kaunti ya Marsabit.
February 7, 2025
Na Naima Abdullahi & Kame Wario,
Mwanamume moja mwenye umri wa makamu ameiaga dunia leo hii baada ya kugongwa na gari katika eneo la kiwanja ndege viungani vya mji wa Marsabit.
Inaarifiwa kuwa mwanaume huyo alikuwa kando mwa barabara kwa nia ya kuvuka barabara wakati gari la kibinafsi lilokuwa likitoka mjini Marsabit kuelekea upande wa Moyale lilipomgonga.
Akithibitisha kisa hicho mkurugenzi mkuu katika hospitali ya rufaa ya Marsabit Kussu Abduba amesema kuwa marehemu alifikishishwa katika hospitali ya rufaa akiwa amefariki.
Kussu ametaja kuwa baada ya upasuaji imebainika kwamba mwanaume huyo aliaga dunia kutokana na majeraha aliyoyapa kichwani mwake.
Mwili ya mwandezake umehifadhiwa katika chumba cha kuhifadhi maiti cha hospitali ya rufaa ya Marsabit.