Mwanaume moja wa miaka 38 ameponea kifo baada ya jaribio la kujitoa uhai kwa kujinyonga kutibuka usiku wa kuamkia leo katika kijiji cha Soweto mjini Laisamis kaunti ya Marsabit.
February 7, 2025
Na Caroline Waforo,
Mhudumu moja wa bodaboda ameuawa kwa kupigiwa risasi na watu wasiojukalana usiku wa kuamkia leo alhamisi.
Mwanaaume huyo wa umri wa makamu alipigwa risasi na watu wasiojulika eneo la Manyatta Shrine viungani mwa mji wa Marsabit mida ya saa sita unusu.
Hakuna kitu kilichoibwa katika kisa hicho ikiwemo bodaboda aliyokuwa nayo.
Mwanaume huyo tayari amezikwa katika maakazi yake eneo la Manyatta Shrine.
Itakumbukwa kuwa huduma za bodaboda zilipigwa marufuku mjini Marsabit kuanzia mida ya saa tano usiku hadi saa kumi asubuhi kutokana na kuongeza kwa visa vya uhalifu.