Local Bulletins

Wazazi katika kaunti ya Marsabit watakiwa kuwachunga wanao wasipate unene wa kupindukia

Na Muchai Joseph

Wazazi karika kaunti ya Marsabit wametakiwa kuwachunga wanao wasije wakapata uzito wa kupindukia. Akiongea na kituo hiki naibu mwalimu mkuu wa shule ya msingi ya SKM Ruth Lekesike amewataka wazazi kuhakikisha kuwa wanao wanapata muda wa kucheza na kufanya mazoezi ili kuwakinga na unene uliopindukia.

Wakati uohuo Bi Lekesike amewataka wanafunzi kujihusisha na shughuli za kuchangamsha viungo vya mwili ili kuboresha afya kwani muda mwingi watoto wengi wamekuwa wakijihusisha na kutazama runinga na simu za mkononi swala linalowanyima nafasi ya kufanya zoezi muhumu kwa afya.

Haya yanajiri huku uchunguzi ukionesha kuwa kwa sasa watoto wengi humu nchini wana unene wa kupindukia yani ujalivu.

Subscribe to eNewsletter