Local Bulletins

Wakulima wanufaika  kaunti ya Marsabit  kwa kupata vyandarua vya kustahimili makali ya jua shade nets..

Na Sabalua Moses

Wakulima kaunti ya Marsabit  wamenufaika na mradi wa kaunti kupitia idara ya kilimo pamoja na shirika la chakula ulimwenguni WFP ya kuwapa mafunzo pamoja na vyandarua vya kustahimili makali ya jua  yaani shade  nets.

Akizungumza na shajara ya radio jangwani mjini Marsabit kaimu mkuu  katika idara ya ukulima Wako Denge Halake amesema  kuwa vifaa hivyo vimeweza kusaidia wakulima sitini katika kaunti hii pamoja na mafunzo ili kuboresha ukulima  pamoja na kukuza  ukulima endelevu.

Vile vile, Wako amesema kuwa vyandarua hivyo kwa vitasaidia   wakulima kukabiliana na makali ya jua pamoja na mabdiliko ya tabia nchi kaunti ya Marsabit.

Wakati huo huo Wako amewahimiza wakulima kupanda mimea ambayo inaweza kustahamili ukame  haswa wakati huu wa mvua

 

Subscribe to eNewsletter