Local Bulletins

Wakaazi katika kaunti ya Marsabit wahimizwa kukuza ufugaji wa nyuki haswa wakati huu wa kiangazi

NA MOSES SABALUA

Wakaazi wa Marsabit wamehimizwa kukuza ufugaji wa nyuki kwani ina manufaa makubwa kwa jamii. Hayo ni kulingana naye Sisaye Bobgala ambaye ni mpatanishi wa shirika lisilokuwa la  kiserikali   la Inua Dada na mfugaji wa nyuki.

Akizungumza na kituo hiki mjini Marsabit  Sisaye Bobgala  amewataka haswa vijana wajiunge na ufugaji  huo wakati huo ambapo kuna mabadiliko ya tabia nchi.

Vile vile  Sisaye amesema ufugaji wa nyuki una faida mno na imeweza kukimu mahitaji ya wakulima wengi katika kaunti ya Marsabit.

Wakati huo  huo amesema kuwa yupo tayari kukuza wakulima wachanga wanaotaka kujisaidia kuanza kuanza ufugaji wa nyuki.

.

Subscribe to eNewsletter