KOSH UNITED KUTOKA KITURUNI NDIO MABINGWA WA TAJI LA NAPO CONSERVATIONS CUP MWAKA WA 2025.
April 25, 2025
Na Sabalua Moses
Huku dunia ikiadhimisha siku ya kifua kikuu (TB) duniani msimamizi mkuu anayesimamia maswala ya kifua kikuu katika kaunti ya Marsabit Bi Sore amesema kuwa visa vya ugonjwa huo katika kaunti ya Marsabit vimeongezeka tangu mwaka jana, huku akiwataka wakaazi kuwa mstari wa mbele kuenda kupimwa na kupata matibabu pindi wanapohisi joto jingi mwilini, ama kukohoa kwa sana.
Hata hivyo Bi Sora amesema asilima 11 ya wale wameathirika na ugonjwa huo ni watoto huku akiwahakikishia wagonjwa kuwa idara yake imeimarisha dawa za kupambana na ugonjwa huo wa kifua kikuu.
Aidha, Bi Sora amesema kuwa chanzo kikuu cha ugonjwa wa kifua kikuu ni ukosefu wa lishe bora pamoja na ukosefu wa hewa safi manyumbani.
Vile vile Bi sora amewataka wakaazi kuwaacha unyanyapaa kwa wagonjwa hao akisema TB ina tiba.
Wakati huo huu Bi sora ameitaka serikali ya kaunti ya Marsabit pamoja na mashirika yasiyokuwa ya kiserikali kusaidia katika kupambana na makali ya ugonjwa huo wa kifua kikuu huku akiwahakishia wagonjwa usalama wao hata baada ya kusitishwa kwa msaada wa shirika la kimarakeni USAID.