Local Bulletins

Vijana kaunti ya Marsabit wahimizwa kutumia mitandao ya kijamii kwa njia inayostahili.

Na Moses Sabalua,

Kufuatia ongezeko la matumizi ya akili mneba almaarufu AI viongozi wa kidini katika kaaunti ya Marsabit wamewataka vijana haswa kuonyesha maadili mema wanapotumia mitandao ya kijamii.

Akizungumza na Shajara Ya Radio Jangwani kasisi katika kanisa la Kenya Assemblies of God (KAG) hapa mjini Marsabit Joseph Mwendwa, amesema kwamba kuwepo kwa teknelojia hiyo kumewasidia watoto pamoja na vijana katika masomo yao  na kuifanya hata  kuwa  rahisi.

Wakati uo huo Kasisi Mwendwa amesema kwamba  teknolojia hiyo pia ina madhara kwani watu wengi hubakia kuwa wavivu  kwani teknolojia hiyo ya  akili mnemba   inawasaidia katika kufanya kazi hizo kwa urahisi.

Vile vile kasisi Mwendwa amewataka vijana kutumia miundo mIsingi yenye maadili mema wanapotumia mitandao ya kijamii ili kuweza kubadilisha maisha ya wanachi.

Subscribe to eNewsletter