Wanafunzi waliokamilisha elimu watakiwa kuwa na subira kuhusu kupokea vyeti vyao vya masomo.
March 25, 2025
Na Moses Sabalua.
Huku ulimwengu ukisheherekea siku ya wanyamapori duniani shirika la kulinda wanyamapori KWS mjini Marsabit walijumuika pamoja na washikadau mbali mbali katika kuadhimisha siku hiyo katika kaunti ya marsabit hii leo.
Akizungungumza na wanahabari mjini marsabit Msimamizi mkuu wa KWS Agostin Ajuoga amesema kuwa lengo kuu la siku hii ni kuwekeza katika jamii kwani kuna umuhimu wa kulinda wanyama pori ikizingatiwa ina manufaa kwa jamii pakubwa pamoja na nchi kwa jumla.
Vile vile Justin Aoga amesema ni sharti jamii ielewe umuhimu wa wanyamapori pamoja na misitu huku akiwataka jamii katika kaunti ya Marsabit kuwa mstari wa mbele kulinda misitu pamoja na wanyamapori.
Aidha Ajuoga ameitaka jamii inaoishi pamoja na wanyamapori kufahamu umuhimu wa kuwatunza wanyamapori hao na vile vile kutafuta namna ya kujisajili kama maeneo ya kuwahifadhi hao wanyama.
Wakati uo huo Ajuoga ameaomba washikadau mbali mbali kushirikiana kwa pamoja ili kusaidia jamii katika kulinda wanyamapori katika kaunti ya Marsabit huku akiwataka walioathiriwa na wanyamapori kuripoti kesi za mashambulizi ya wanyamapori kwa shirika hilo la KWS.