Local Bulletins

Mifugo wasombwa na mafuriko katika eneo bunge la North Horr kufuatia mvua kubwa iliyonyesha hapo jana.

Na Caroline Waforo,

Idadi ya mifugo isiyojulikana walisombwa na mafuriko katika eneo bunge la North Horr kufuatia mvua kubwa iliyonyesha hapo jana.

Haya ni kulingana na kamishana wa kaunti ya Marsabit James Kamau ambaye amezungumza na wanahabari leo hii afisini mwake.

Kamishna Kamau amewataka wakaazi jimboni na haswa walio katika maeneo yanayoshuhudia mvua kuchukua tahadhari kwa kuepuka sehemu ambayo maji hupitia ili kuepuka hatari iwapo mvua itaendelea kunyesha.

Subscribe to eNewsletter