Local Bulletins

Kuna umuhimu wa kufunza wanafunzi lugha ya kifaransa katika  mfumo wa C.B.C wasema wataalam wa elimu.  

Huku wataalamu  wa  elimu wakipongeza   mfumo wa elimu chini ya C.B.C baadhi ya watalaam hao  katika kaunti ya Nairobi wamesema kufunza wanafunzi lugha ya kifaransa  shuleni ina umuhimu kwani itasaidia katika  kuboresha sekta ya biashara , elimu pamoja  na mahusiano ya  kidiplomasia .

Aidha ,katika kaunti ya  marsabit wazazi wametoa  maoni yao kulingana na pendekezo  hilo la kutaka   kuwafunza wanafunzi  somo la kifaransa katika elimu mpya ya C.B.C wakidai kuwa  cha muhimu ni kuwafunza lugha ambazo zinakuzwa  katika taifa letu.

Wakizungumza na kituo hiki baadhi  yao wamesema kuwa  cha msingi ni kuendeleza masomo ya C.B.C  huku wakikitaka ufafanuzi wa kutosha  haswa katika kuenzi masomo  ya C.B.C

Wakati huo huo , baadhi yao wamesema kuwa ipo  umuhimu wa  kufunza wanafunzi hao  lugha nyingine  na  sio tu lugha ya kifaransa ili kukuza utamaduni wao.

Pia  baadhi  ya wazazi mjini marsabit wamepinga himizo hilo   wakisema ni sharti wajumuishe lugha ya mama  pamoja na mila katika mfumo wa C.B.C kwani ina manufaa kwa wanafunzi hao..

Subscribe to eNewsletter