Local Bulletins

Itakua vigumu kwa rais Ruto kupata muhula wa pili iwapo hatatimiza ahadi zake

BAADHI ya wakaazi Jimboni Marsabit wamepinga kauli ya Rais William Ruto, ambaye amedai kwamba yuko tayari kukabiliana na upinzani wowote mwaka wa 2027, akisisitiza kuwa utendajikazi wake utafanikisha muhula wa pili.

Wakaazi hao wamesema hawaoni matokeo yoyote kutoka kwa utendakazi wa Rais Ruto, na wanataka mabadiliko ya kweli katika uongozi wake.

Wamesema wanatarajia kuona maendeleo ili kuboresha maisha yao, badala ya ahadi zisizotekelezeka.

Wakaazi hao wamehimiza viongozi wao kuzingatia maslahi ya jamii na kuhakikisha kwamba huduma muhimu zinapatikana.

Subscribe to eNewsletter