Wizara ya afya Marsabit ndio iliyotengewa mgao mkubwa, Zaidi ya 30% kwenye makadirio wa kifedha 2025/26
June 20, 2025
Caroline Waforo,
Pendekezo la waziri wa Usalama wa ndani Kipchumba Murkomen la machifu walio katika maeneo hatari kupewa bunduki ili kujilinda linaendelea kupongezwa haswa na machifu.
Wa hivi punde ni chifu wa lokesheni ya Jirime Chifu Enock Kallo ambae ameunga mkono mpango huo akisema kwamba utawasaidia kujilinda.
Chifu Kallo ameitaja hatua hiyo kama itakayohakikisha kwamba machifu pia wako salama na kuwaepusha na mashambulizi ambayo huelekezwa kwao kutokana na majukumu yao.
Mpango huo unahusisha machifu kutoka kunti za Marsabit, Isiolo, Meru, Laikipia na Samburu.
Hii ni baada ya machifu kukiri kuwa wanawafahamu wezi wa mifugo ila wanahofia kuwakamata kutokana na uwoga wa kuvamiwa.