Wanaharakati waitaka serikali kuharakisha mchakato wa kutuma pesa za kufadhili masomo ili kunusuru wanaofukuziwa karo.
May 16, 2025
Na Caroline Waforo,
Maafisa wa polisi pamoja kwa ushirikiano na machifu wanaendeleza msako wa pombe haramu pamoja na mihadarati mjini Marsabit.
Operesheni hiyo iliyongo’a nanga alhamisi wiki jana inapania kuhakikisha kuwa utumizi wa pombe haramu pamoja na mihadarati unakomeshwa kikamilifu kulingana na kamanda wa polisi Leonard Kimaiyo.
Aidha wamiliki wa vilabu wametakiwa kutii sheria kwa kuhakikisha kuwa vilabu hivyo vinafunguliwa saa kumi na moja jioni na kufungwa saa tano usiku.
Anasema kuwa watakao kamatwa wakikiuka sheria watawajibishwa kwa mjibu wa sheria.