Local Bulletins

Mkuu wa Utumishi wa Umma: Joseph Kinyua aondoka rasmi na kumpisha Felix Kosgei

Na Machuki Dennson

Rais William Ruto amempongeza Kinyua kwa utendakazi wake katika afisi yake.

Rais amesema kuwa Kinyua amehakikisha kumekuwa na mpito salama na mzuri kama inavyofaa katika taifa lenye uchaguzi wa demokrasia.

Felix Kosgei amekjula kiapo na kuanza kuhudumu mara moja kama mkuu wa utumishi wa umma katika ikulu ya rais.

 Kosgei anachukua nafasi hiyo kutoka kwake Joseph Kinyua ambaye amehudumu katika afisi hiyo kwa miaka 10.

Kosgei amelishwa kiapo na Kinyua ambaye amestaafu baada ya muda wake wa kuhudumu kukamilika.

Naibu wa Kosgei sasa atakuwa aliyekuwa gavana wa Turkana Josphat Nanok.

Kosgei aliwahi kuhudumu kama wazoro wa kilimo kati yam waka 2013 hadi mwaka 2015 wakati alilazimika kujiuzulu kwa sababu ya sakata za ufisadi. Kosgei ameanza kuhudumu mara moja kwa kuwalisha kiapo mawaziri wapya mbele ya rais William Ruto.

Subscribe to eNewsletter