Local Bulletins

Shirika La Chakula Duniani FAO Lasema Kuwa Liko Tayari Kusaidia Serekali Ya Kenya Kupambana Na Nzige.

Picha; Hisani

By Waihenya Isaac

Huku serekali ikiendelea kuhakikisha kuwa miradi yake inakamilika kabla ya rais Uhuru Kenyatta kuondoka mamlakani,Msemaji wa serekali Kanali Cyrus Oguna amezuru kaunti za Meru na Isiolo ili  kutadhimini juhudi za kupambana na nzige wa Jangwani.

Akizungumza Katika eneo la Burati kaunti ya Isiolo, Oguna amesema kuwa serekali itafanya kila iwezalo ili kupambana na wadudu hao waharibifu ambao wanahatarisha uzalishaji wa chakula.

Aidha shirika la chakula duniani FAO limesema kuwa liko tayari kusaidia serekali kupambana na nzige hao.

Itakumbukukwa kuwa baada ya kuingia Ofisini kwa mhula wa pili serekali ya Jubille iliahidi kutekeleza ajenda nne kuu za serekali huku utoshelevu wa chakula ikiwa ni  mojawapo ya ajenda hizo.

Subscribe to eNewsletter