Local Bulletins

Mwanamume Mmoja Aaga Dunia Wakti Akichimba Kisima Katika Eneo La Alamanu Mji Wa Mararal Kaunti Ya Samburu.

Kisima Cha Maji Katika Kaunti Ya Samburu.
Picha; Hisani.

By Waihenya Isaac,

Mwanamume mmoja ameaga dunia wakti akichimba kisima katika eneo la Alamanu mji wa Mararal katika kaunti ya Samburu.

Akidhibitisha kisa hicho Kamanda wa polisi katika kaunti ndogo ya Samburu ya kati Alex Rotich amesema kuwa huenda marehemu alifariki kutokana na matatizo ya kupumua kabla afike mwisho wa kina cha kisima.

Maafisa wa polisi wakishirikiana na wananchi walichukua zaidi ya saa sita kutoa mwili huo kutoka ndani ya kisima hicho bila mafanio hadi mwendo wa saa tisa alasiri wakti ambapo juhudi zao zilizaa matunda.

Mwili wa maheremu umehifadhiwa Katika chumba cha kuhifadhi maiti katika hospitali ya rufaa ya Samburu.

Kisa hicha ni cha pili cha mtu kupoteza maisha Katika juhudi za kukarabati kisima Katika eneo hilo.

 

Subscribe to eNewsletter