Local Bulletins

Mitihani Ya Kitaifa Itaendelea Kama Ilivyopangwa – Asema Waziri Magoha

Waziri wa Elimu Profesa George Magoha.
Picha;Hisani

By Waihenya Isaac,

Mitihani ya kitaifa itaendelea kama ilivyopangwa.

Kwa mujibu wa waziri wa elimu Nchini Profesa George Maghoha ni kuwa serekali haipanii kuahirisha mitihani hiyo hata licha ya washikadao Katika sekta elimu kutaka mitihani hiyo kuahirishwa kwa vigezo kuwa watahiniwa hajajiandaa kikamilifu.

Akizungumza Katika shule yamsingi ya Mwiki Katika eneo la Githurai kaunti ya Nairobi alikofika kutadhimini hali ya masomo shuleni,Maghoa amewataka wazazi kutohofia kuhusiana na swala la mitihani hiyo huku akisema kuwa serekali imeshughulikia matakwa yote.

Aidha waziri maghoha ameahidi kuwa serekali itasambaza dawati kwa shule ambazo hazikuwa zimepokea dawati hizo ili kufanikisha elimu.

Vilevile amesisitiza kuwa wazazi wataghamirikia hasara itakayosababishwa na wanafunzi shuleni huku waalimu wa zamu wakiwajibishwa kikamilifu.

Subscribe to eNewsletter