Local Bulletins

Maafisa Wa Polisi Kutoka Kambi Ya Mafunzo Ya Kedong Na OCPD Wa Naivasha Waharibu Zao La Bhangi Lenye Thamani Ya Sh Milioni 27.

Picha;Hisani

By Samuel Kosgei,

Kitengo cha maafisa wa upelelezi wa kukabiliana na dawa za kulevya, maafisa wa polisi kutoka kambi ya ya mafunzo ya  Kedong na OCPD wa Naivasha wameharibu zao la bhangi lenye thamani ya Sh Milioni 27.

Washukiwa 14 ambao walipatikana wakipalilia bhangi hiyo kwenye shamba la zaidi ya ekari moja katika eneo la Kedong, pia wamekamatwa na kutiwa mbaroni, huku uchunguzi zaidi ukiendelea.

Kukamatwa kwao kulifuatIa ujumbe kutoka kwa kwa umma, ambao walitoa habari kuhusu shamba hilo kwa kupiga simu kwa DCI.

Subscribe to eNewsletter