Local Bulletins

Ibada Ya Wafu Ya Mamake Kinara Wa ANC Musalia Mudavadi, Hannah Atsianzale Mudavadi Yaandaliwa Hii Leo Jijini Nairobi.

Ibada Ya Wafu Ya Mamake Kinara Wa ANC Musalia Mudavadi,Hannah Atsianzale Mudavadi Yaandaliwa Jijini Nairobi.
Picha; Hisani

By Waihenya Isaac.

Ibada Ya Wafu Ya Mamake Kinara Wa ANC Musalia Mudavadi, Hannah Atsianzale Mudavadi Inaendela Katika Kanisa La Friends Ngong Jijini Nairobi.
Atsianzale Aliaga Dunia Disemba 28, 2020 Alipokuwa Akipokea Matibabu Katika Hospitali Ya Nairobi Akiwa Na Umri Wa Miaka 92.
Mama Hannah Atsianzale Atapumzishwa Jumamosi Hii Nyumbani Kwake Eneo La Mululu Kaunti Ya Vihiga.
Aidha Viongozi Mbali Mbali Akiwemo Naibu Wa Rais Wiliam Ruto,Aliyekuwa Makamu Wa Rais Kalonzo Musyoka, Spika Wa Bunge La Kitaifa Justin Muturi, Mawaziri Mutahi Kagwe Wa Afya, Eugine Wamalwa Wa Ugatuzi, Maseneta Pamoja Na Wabunge Zaidi Ya 20.
Siasa Za Chaguzi Ndogo Zinazotarajiwa Kuandaliwa Mwezi Machi Mwaka Huu Hazikusazwa Katika Hafla Hiyo Huku Mbunge Wa Kimilili Chris Wamalwa Akivitaka Vyama Vingine Kutowasimasisha Wagombea Katika Ngome Za ANC Na FORD Kenya.
Siasa Za Mulembe Nation Pia Zimesheheni Katika Hafla Hiyo Huku Viongozi Wakitaka Jamii Hiyo Kuja Pamoja Na Kuwania Uongozi Wa Taifa Katika Uchaguzi Mkuu Wa Mwaka Wa 2022.

Subscribe to eNewsletter