Local Bulletins

Hatma Ya Walimu Zaidi Ya Elfu 300 Walio Na Cheti Cha P1 Ambao Hawajaajiriwa Haijulikani Baada Ya Serikali Kuogeza Vigezo Vya Kufuzu Na Cheti Hicho.

Picha; Hisani

By Samuel Kosgei,

Hatma Ya Walimu Zaidi Ya Elfu 300 Walio Na Cheti Cha P1 Ambao Hawajaajiriwa Haijulikani Baada Ya Serikali Kuogeza Vigezo Vya Kufuzu Na Cheti Hicho.

Mwezi May Mwaka Huu Vyuo Vya Kutoa Mafunzo Kwa Walimu Vinatarajiwa Kuanza Kutoa Huduma Za Diploma Pekee Ili Kuwiana Na Mtalaa Mpya Wa CBC.

Hiyo Inamaanisha Kuwa Walimu Wanaotaka Kufundisha Shule Za Msingi Lazima Wawe Na Diploma (DPTE) Badala Ya P1 Kama Ilivyo Kwa Sasa.

Kundi La Mwisho La Walimu Wanaosomea P1 Wanatarajiwa Kumaliza Mafunzo Mwezi Machi Mwaka Huu Ili Watakaofuata Wasomee Cheti Cha Diploma.

Watasomea Cheti Hicho Kwa Kipindi Cha Miaka Mitatu Badala Ya Miwili Kama Ilivyokuwa.

Hatua Hii Huenda Ikawa Faida Kwa Watakaokuwa Na Diploma Kwani Itakua Rahisi Kupata Kazi Pindi Tu Baada Ya Kufuzu Na Pia Kurahisishia Kazi Tume Ya TSC Na Taasisi Ya Mtaala KICD Ambayo Imekuwa Ikitoa Mafunzo Ya CBC Kwa Walimu Walioajiriwa.

Subscribe to eNewsletter