Local Bulletins

Gavana Wa Kaunti Ya Kakamega Wycliffe Oparanya Amtaka Kinara Wa ODM Raila Odinga Kuunga Mkono Azma Yake Ya Kuwania Urais Mwaka 2022.

Gavana Wa Kaunti Ya Kakamega Wycliffe Oparanya.
Picha; Hisani

By Waihenya Isaac,

Gavana wa Kaunti ya Kakamega Wycliffe Oparanya ameelezea matumaini ya kupata tiketi ya chama cha ODM ili kuwania urais mwaka wa 2022.

Oparanya, ambaye ni Mwenyekiti wa Baraza la Magavana nchini, amesema atatuma ombi la kuteuliwa ili kujiunga na wale watakaopigania tiketi ya chama hicho ya kuwania urais huku akimtaka kinara wa chama cha ODM raila Odinga kuunga Mkono azma yake.

Adha Oparanya Amesema kuwa kwa sasa taifa linataka kiongozi mwenye maadili na atakaye weza Kufufua uchumi wan chi, huku akitaja kuwa ametimiza vigezo Hivyo.

Tayari chama cha ODM kimewataka wanachama wake kutuma maombi kwa bodi ya kitaifa ya uchaguzi ikiwa wanataka kuwania urais kwa tiketi ya chama hicho kwenye uchaguzi wa urais wa mwaka 2022.

Chama hicho kimesema kuwa wanaotaka kuwania uteuzi huo sharti walipe ada ya shilingi milioni moja kwa akaunti ya benki ya chama hicho.

Subscribe to eNewsletter