Local Bulletins

Bunge La Kaunti Ya Siaya Limepitisha Muswada Wa Marekebisho Ya Katiba BBI.

Bunge La Kaunti Ya Siaya.
Picha:Hisani

By Waihenya Isaac,

Bunge la Kaunti ya Siaya limepitisha Muswada wa Marekebisho ya Katiba BBI ambao utanatajiwa fungua njia kwa kura ya maoni nchini.

Bunge hilo limekuwa la kwanza kuidhinisha mwaada huo uliowasilishwa kwa mabunge ya kaunti na tume huru ya uchaguzi na mipaka Nchini IEBC baada ya kusanifisha Zaidi ya sahihi milini moja za kuunga Mkono mchakato huo.

Spika wa Bunge la Kaunti ya Siaya George Okode amethibitisha matokeo akibainisha kuwa alikuwa akijiandaa kupeleka matokeo kwa Bunge la Kitaifa.

Aidha mswada huo unahitaji kupitishwa na mabunge ya kaunti yapatayo 24 kati ya 47 chini ya muda wa siku 90 ili kukubalisha zoezi la Kura ya maoni kuandaliwa.

Subscribe to eNewsletter